Vijana wa Muleba Wako Uso kwa Uso na Waziri wa Maendeleo ya Vijana
Vijana kutoka Wilaya ya Muleba walipata fursa ya kukutana uso kwa uso na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Arthur Nanauka, wakati wa ziara yake ya kikazi katika mkoa huo.
Katika mkutano huo, vijana walieleza changamoto wanazokabiliana nazo katika shughuli zao za kiuchumi, wajasiriamali na maendeleo ya kijamii. Waziri Nanauka aliwasikiliza kwa makini na kutoa mwongozo pamoja na ushauri kuhusu jinsi ya kutumia fursa za serikali na miradi ya uwezeshaji wa vijana.
Vilevile, aliwahimiza vijana kushirikiana, kubuni miradi yenye tija na kutumia ipasavyo mikopo na programu zinazotolewa na Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana ili kuongeza kipato na kuimarisha maendeleo ya jamii zao.
VIJANA Mkoa wa Singida wanatarajia kunufaika na mikopo isiyokuwa na riba kutoka...
Wajasiriamali Mkoani Singida wameaswa kuziona changamoto zinazowakabili kama fur...
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Maendeleo ya Vijana, Mhe. Joel Arthur Nana...
UN CAREERS LIVESTREAM EVENT 2026 Kwa Wanafunzi wa Vyuo Vikuu na Wahitimu Wapy...
WAZIRI NANAUKA AWEKA MIKAKATI YA KUWAWEZESHA VIJANA NA WANAWAKE KIUCHUMI Seri...